Monday, June 29, 2009

Ulaya sasa kuwa na aina moja tu ya chaja !

UMOJA WA ULAYA umeamua kwamba kuanzia sasa Ulaya yote itakuwa inatumia aina moja tu ya chaja katika kuchaji simu za mkononi.

Uamuzi umefuatilia usumbufu watu wanaoupata katika kutafuta ainay ya chaja inayofaa simu fulani. Matokeo yake ni kwamba kila mwaka mamilioni ya chaja zinazokufa hutupwa na hivyo kuongeza uchafuzi wa hali ya hewa na mazingira duniani.

Kuwepo kwa chaja moja kutapunguza sana wingi wa chaja majumbani, mahotelini, vilabuni, vyuoni, maofisini na sehemu zingine mtu anazolazimika kuwa na chaja.

Chaja mbili tatu zitatosha kabisa zinapokuwepo sehemu husika na wote watakuwa wanachangia ubora wa mazingira yao.

USHAURI: Jadili na wenzako, je, chaja aina moja inahitajika hapa Afrika Mashariki ?

No comments:

Post a Comment